Skip to main content

Posts

TIZAMA TFS WALICHOFANYA MSITUNI

 TFS YASHIRIKI KIKAO CHA UWEKEZAJI KUTANGAZA UTALII WA MISITU. Akizungumza kwa niaba ya Kamishina wa Uhifadhi TFS Profesa Dos Santos Silayo tarehe 17/05/2022 jijini Dar es salaam Mhifadhi Mkuu Zainabu Bhungwa amesema kikao hicho kati ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na utalii Mh Juma Selemani Mkomi na Wawekezaji kutoka Ufaransa utaleta tija katika kuutangaza utalii wa Misitu.  Bi Zainabu amesema kupitia kikao hicho TFS imepata nafasi ya kuwaeleza wawekezaji hao fursa za uwekezaji kwenye Vivutio vya Utalii vinavyosimamiwa na TFS.  "Kikao hiki ni muhimu kwa TFS, tumeweza kuwaeleza Wawekezaji fursa za kuwekeza kwenye Vivutio vyetu, kama ilivyo kwa Mheshimiwa Rais kupitia filamu ya Tanzania The Royal tour anavyotangaza utalii, sisi TFS pia tunamuunga mkono kupitia Vivutio vyetu vya Utalii kwenye Hifadhi za Misitu." Bi Zainabu.  Awali katika kikao hicho Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na utalii Mh Juma Selemani Mkomi amewakaribisha wawekezaji hao na kuwahakikishia ku
Recent posts

WACHIMBAJI MADINI WAPIGWA MSASA

 TUME YA MADINI YAWAPIGA MSASA WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI KUHUSU USIMAMIZI WA AFYA, USALAMA, BARUTI NA SHERIA ZA MADINI  KWENYE UCHIMBAJI MADINI MIRERANI Timu ya wataalam waandamizi wa Tume ya Madini wakiongozwa na Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Migodi na Mazingira, Mhandisi Henry Mditi wameendelea kutoa mafunzo kwa wamiliki wa migodi, wachimbaji wadogo wa madini na wasimamizi wa baruti kuhusu usimamizi wa afya, usalama, baruti na sheria za madini katika eneo la Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara. Katika mafunzo hayo ambayo awali yamezinduliwa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba mada zilizotolewa ni pamoja na sheria ya madini na kanuni kuhusu eneo tengefu la Mererani na uchimbaji salama migodini. Mada nyingine ni pamoja na utunzaji wa mazingira migodini na usimamizi wa baruti migodini. Wakizungumza katika nyakati tofauti wadau wa madini waliohudhuria mafunzo hayo wameipongeza Tume ya Madini kwa utoaji wa elimu safi na kushauri elimu kuendelea kutolewa kwenye

MBIO ZA MWENGE DAR ES SALAAM

  RAS RUGWA  APOKEA MWENGE WA UHURU KUTOKA  MKOA WA PWANI *- Ataja ratiba ya Mwenge kukimbizwa Dar es Salaam* *-Asisitiza Umuhimu wa Mwenge huu, Kauli Mbiu na Ujumbe wake* *- Ataja thamani ya Miradi itakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru* *-Akabidhi  Mwenge huo kwa Mkuu wa Wilaya Kinondoni ambapo DC huyo akiri kuupokea na kuukimbiza katika Wilaya yake* Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam *Ndg. Hassan Rugwa* amepokea Mwenge wa Uhuru Leo tarehe 10 Aprili 2022 katika Uwanja wa Shule ya Msingi Bunju "A" ukitokea Mkoa wa Pwani Baada ya kuupokea Mwenge huo wa Uhuru *Ndg. Hassan Rugwa* ametaja ratiba ya ukimbizwaji wa  Mwenge katika Mkoa wa Dar es Salaam kuwa tarehe 10/05/2022 Utakimbizwa Kinondoni, tarehe 11/05/2022 Utakimbizwa Ubungo, tarehe 12/05/2022 Ilala, tarehe 13/05/2022 Kigamboni na kumalizika Temeke tarehe 14/05/2022 ambapo tarehe 15/05/2022 utakabidhiwa *Mkoa wa Kusini Pemba* Aidha *Katibu Tawala* amesisitiza Umuhimu wa Mwenge  wa Uhuru wa 2022 unaosisitiza Sensa ya Watu na

Mhe. Dr Seleman Jafo aipongeza Wilaya ya Bahi

  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo ameipongeza Wilaya ya Bahi kwa kutekeleza maelekezo ya Serikali ya upandaji miti kwa wanafunzi. Ametoa pongezi hizo leo Mei 7, 2022 wakati aliposhuhudia utiaji saini wa makubaliano ya upandaji miti kati ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi na walimu wakuu wa shule za msingi uliokwenda sambamba na Bonanza la Walimu wilayani humo. Dkt. Jafo amesema kuwa hatua ya kusaini mkataba huo itaongeza hamasa kwa walimu kuwasimamia wanafunzi katika shule zao kushiriki kikamilifu katika zoezi la upandaji wa miti. Alisema tuna kila sababu ya kuifanya nchi yetu kuwa ya kijani na ndiyo maana Januari 22, 2022 ilizinduliwa kampeni ya utunzaji wa mazingira kwa wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na vyuo ‘Soma na Mti’ lengo likiwa ni kuweza kupata miti mingi zaidi sambamba na maelekezo ya Serikali kwa kila halmashauri kupanda miti milioni 1.5. “Niwapongeze sana Bahi leo mnasainiana mikataba baina ya Mkuu wa Wilaya na walimu k

TANESCO KUOKOA TAKRIBANI 1.7 BILIONI NGORO NGORO

TANESCO KUOKOA TAKRIBANI BIL.1.7 NGORONGORO Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la Umeme nchini (TANESCO) imekamilisha ujenzi wa mradi wa umeme wenye thamani ya shilingi bil. 2.9 wa kuunganisha Wilaya ya Ngorongoro kwenye grid ya taifa. Awali Wilaya ya Ngorongoro ilitumia umeme wa jenereta ambao ulikuwa ukigharimu kiasi cha bil.1.7 kama gharama za uendeshaji kwa mwaka,huku makusanyo ya wilaya ya ngorongo yakiwa ni Mil.374 kwa mwaka. Akizindua umeme  huo wa gridi katika Wilaya ya Ngorongoro  Halmashauri ya mji mdogo wa Loriondo Mei 06, 2022, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe:John Mongela amesema TANESCO imekuwa ikifanya kazi kubwa katika kuwafikishia huduma ya umeme wananchi na uboreshaji wa miundombinu. "Leo tunapozindua umeme gridi ya Taifa ni ushahidi tosha wa kazi kubwa wanayoifanya TANESCO, tumeona mradi huu ukikamilika ndani ya muda mfupi" amesema Mhe. Mongela. Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Arusha, Mhandisi Herini  Mhina amesema mradi

MBIO ZA MWENGE ZATUA KISARAWE

MWENGE WA UHURU WAFUNGUA MIRADI KISARAWE WAZIRI DR JAFO AWAPONGEZA VIONGOZI KISARAWE DC,DED WAPOKEA UFAFANUZI WA MWENGE KUYATEKELEZA KWA WAKATI ULIOPANGWA  NA....., PWANI-KISARAWE Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2022 Ndg  SAHIL NYANZABARA GERARUMA amefungua miradi ya maendeleo mbalimbali kumi na mbili iliyopangwa katika wilaya ya kisarawe katika  miundombinu ya barabara,afya,elimu, maji,vijana mikopo na uwezeshaji* Mwenge wa uhuru umekuja kisarawe kumulika maendeleo ambayo viongozi wa serikali wanayasimamia kwa mujibu wa Sheria miradi ambayo wamepatiwa fedha za serikali kuja kwenu kwa ajili ya maendeleo ya jamii kwa ujumla, *Serikali inawaletea maendeleo nyie wananchi katika sekta ya miradi ya Afya,Maji Elimu na miundombinu mbalimbali ili kupata urahisi wa maisha hivyo ni lazima wananchi kushiriki kuyajua haya ili kuwasimamia viongozi wetu na swala la kujua miradi katika Kijiji ni lako mwananchi alisisitiza Geraruma* Hata hivyo nae mbunge wa Jimbo la kisarawe ambaye pia wazir

Tutamkumbuka Dr. Mahiga

Dk Augustine Mahiga alizaliwa Agosti 28, 1945 huko Tosamanganga, Jimbo la Kalenga, mkoani Iringa (angetimiza miaka 77 ifikapo Agosti mwaka huu). Amesoma elimu ya msingi katika shule za Serikali enzi ya mkoloni na alihitimu darasa la VIII muda mfupi baada ya uhuru. Safari ya elimu ya Dk Mahiga ilikuwa ya umaskini uliopitiliza, alishindwa kuendelea na elimu ya sekondari kwa kutokuwa na fedha za kulipia mashuka na mablanketi hadi aliposaidiwa na msamaria mwema kutoka Shirika la Kennedy wakati huo. Aliendelea na masomo ya sekondari hapahapa nchini na mwaka 1968, alijiunga katika Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki, Dar es Salaam na kuhitimu Shahada ya Sanaa akibobea kwenye elimu mwaka 1971. Mwaka huohuo, Dk Mahiga alipata ufadhili na kuendelea na masomo ya juu nchini Canada katika Chuo Kikuu cha Toronto ambako alihitimu Shahada ya Uzamili. Aliendelea na masomo ya Shahada ya Uzamivu (PhD) katika chuo hichohicho akijikita katika Uhusiano wa Kimataifa na kuhitimu mwaka 1975. Mwaka huohuo 1975 (ak